Posts

Showing posts from July, 2021

SHANTA GOLD YAPATA PONGEZI KUSIMAMIA LOCAL CONTENT

Image
Na Mwandishi wetu Singida: Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko ameeleza kuwa, Mgodi Mpya wa Kati wa Dhahabu wa Shanta ndio Mgodi pekee Tanzania unaotekeleza ipasavyo Matakwa ya Sheria ya matumizi kwa Jamii husika (Local Content). Amesema hayo tarehe 30 Julai, 2021 baada ya kutembelea na kukagua Maendeleo ya Ujenzi wa Mgodi wa Kati wa Dhahabu wa Shanta Singida (SINGIDA GOLD MINE) ambao upo Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida. Amesema historia ya ujenzi wa Mgodi huo, kwa miaka mitano yote iliyopita Mgodi wa Shanta ndio Mgodi wa Kati mpya uliojengwa hapa Nchini kwa muda mfupi. Akizungumzia kuhusu umuhimu wa Sheria ya Local content Waziri Biteko amesema katika uwekezaji inawahitaji Wawekezaji wakubwa, wa kati na wadogo ili kufanya uchumi uwe na maana. “Kama biashara wafanye wenyeji, tulikuwa na Migodi ambayo hata nyama ilitoka South Africa, lakini Mgodi ambao mwaka huu tumewapa tuzo ya Local content, huu ndio mgodi ambao asilimia 100 ya walioajiriwa ni watanzania" ameeleza Biteko. Aidha, am

SUPHIAN JUMA ATO YA MOYONI KUFARIKI KWA ALIYEKUA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO Bi. ANNA ELISHA MGHWIRA.

Image
ANNA ELISHA MGHWIRA, SIASA SAFI, MAMA MWEMA ANAYEISHI MIOYONI MWA WATU. Ukiachana na Televisions kadhaa ambazo nilizowahi kufanya nazo kazi, mitandao ya kijamii imenisaidia kwa asiliamia zaidi ya 90 kunikutanisha na watu maarufu, na muhimu katika Taifa letu. Kwangu mimi Suphian, Mitandao ya kijamii ni Ofisi kama Ofisi zingine za watu wengine. Matokeo ya matumizi chanya ya mitandao ya kijamii ndiyo yaliyonikutanisha na Mgombea wa Kwanza Mwanamke wa kiti cha Urais Tanzania, Mama Anna Elisha Mghwira. Nakumbuka ilikuwa mwaka 2015 pale Makumbusho Dar, kwenye Mkutano Mkuu wa ACT wazalendo ambapo Mama Anna kama Mwenyekiti wa Chama hicho baada ya kutoa hotuba kwa wagombea Ubunge wa Chama hicho, ndipo tulikutana na kuzungumza mambo kadhaa kuhusu siasa za Taifa na kipekee siasa za Singida kwani mimi na yeye ni wazawa wa Mkoa wa Singida na Kabila moja la Kinyaturu. Wajibu wangu wa kwanza ulikuwa ni kumsaidia katika kufungua, kusimamia na kuziendesha akaunti/kurasa zake za mitandao ya kijamii. Wa

ZIARA YA MBUNGE WA JIMBO LA SINGIDA MASHARIKI MHE. MIRAJI MTATURU JIMBONI

Image
Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Mhe Miraji Mtaturu Leo tarehe 19 July, 2021 amefanya ziara kata ya Siuyu baada ya kutembelea Miradi shule ya Sekondari Siuyu aliwapelekea Milion 3 kuendeleza ujenzi wa maabara na serikali imepeleka milion 30 kumalizia ujenzi huo. Serikali imepeleka milion 40 kujenga vyumba viwili vya madarasa na ofisi ya walimu. Serikali imepeleka milion 12 kujenga madarasa shule ya msingi Nalli,matundu ya vyoo 6 zahanati ya Unyankhanya ujenzi wa matundu 6 ya vyoo. Nimewajulisha rasmi wananchi wa Siuyu serikali imetenga milion 280 kufungia barabara muhimu ya Siuyu-Nalli-Makotea km 7.26 inayounganisha vijiji vya kata ya Siuyu. #SingidaMashariki#MaendeleoYetu#KipaumbeleChetu#KaziIendelee#

TAARIFA MUHIMU KWA WANANCHI WA JIMBO LA SINGIDA MASHARIKI

Image
Nawasalimu kwa Jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Napenda kutoa taarifa rasmi kwa wananchi wa *Jimbo la Singida Mashariki* kuhusu Bajeti ya *Mwaka 2021/22* kwenye Jimbo letu *,Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Mama Samia Suluhu Hassan* imetutengea *Tsh Bilion 1.5* kwa ajili ya kufungua Barabara mpya ambazo hazijawahi kufunguliwa kabisa,Ujenzi wa madaraja na kuziimarisha zilizopo ili kurahisisha mawasiliano ndani ya Jimbo pamoja na shughuli za kiuchumi. Hatua hiyo ni utekelezaji wa *Ilani yetu ya CCM 2020- 2025* ambayo pamoja na mambo mengine imeahidi kuendeleza shughuli za ujenzi wa miundombinu mbalimbali Ili kuifanya sekta hiyo ifikie malengo yake ya kuwezesha wananchi kuendelea na uzalishaji kwa ajili ya kuongeza kipato chao. Hivyo Basi, Baada ya kushauriana na Meneja wa TARURA tumekubaliana Barabara zifuatazo zitengenezwe; 1.Misughaa-Msule-Sambaru km 27.90 Tsh Milioni 600. 2.Mungaa-Ntuntu-Mang'onyi km 15 Tsh milion 330. 3.Siuyu-Nali-Makotea km 7.26 Tsh Mili

KINGU NA WANANCHI WA JIMBO LA SINGIDA MAGHARIBI, MIUNDOMBINU YA BARABARA JIMBONI

Image
Na Elibariki Kingu (Mb) Napenda kuwataarifu Wananchi wote wa Jimbo la Singida Magharibi; kuwa. Serikali ya CCM inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imeshaelekeza TARURA Mikoa na Wilaya kuainisha Barabara zitakazo jengwa kwa nyongeza ya bajeti ya Tshs Bilion moja tuliyopewa. Barabara zetu za Jimbo la Singida Magharibi zitakazojengwa kwa kiwango Cha MORAMU ni kama ifuatavyo:- 1. Barabara ya Isuna - Ngo’ngosoro hadi Ilolo KM 8. Milion 250: jina la Barabara haimaanishi tunajenga upande wa isuna hadi Ng'ongosoro hapana, bali ni upande wa Singida Magharibi unaopakana na Ngo’ngosoro. Lengo ni watu wetu wafike Ikungi bila kuja mpaka puma na barabara hii ni muhimu kwa uchumi wa watu wetu: 2. Mtamaa -Minyughe - Mtavira urefu KM 4 na daraja lililokatika huko Makilawa milioni (330M:) haimaanishi tutajenga mtamaaa maana ni ya mjini bali ni jina la barabara, pesa zitatumika kujenga upande wa Kata ya Minyughe na Makilawa, Barabara hii ni muhimu sana kwa uchumi wa Kata hizi mbili kwa usafirish