Posts

MTATURU AITAKA SERIKALI KUJENGA SOKO LA KISASA MAKAO MAKUU YA WILAYA YA IKUNGI

Image
na Bazil Mjungu: Dodoma MBUNGE wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu ameihoji serikali ni lini itatenga fedha kwa ajili ya kujenga soko la kisasa wilayani Ikungi Mkoani Singida. Mtaturu ameuliza swali hilo April 24,2023, Bungeni Jijini Dodoma. Akijibu swali hilo, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Dr Festo Dugange amesema Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi imeweka mpango wa kujenga soko la kisasa katika Kijiji cha Ikungi lenye ukubwa wa Ekari 2. Amesema kwa sasa Halmashauri inaendelea kufanya mazungumzo na wananchi ambao wamejenga vibanda vya biashara katika eneo hilo lililoainishwa na mipango miji kwa ujenzi wa soko la kisasa. "Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi kwa kushirikiana na UN WOMEN imekamilisha ujenzi wa jengo la mabucha na mbogamboga lenye thamani ya shilingi Milioni 82 katika eneo hilo,"amesema. Aidha, ameahidi kuwa serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa soko la kisasa Ikungi.

MILIONI 300 ZIMELETWA KUJENGA MABWENI SHULE YA MSINGI IKUNGI MCHANGANYIKO: MTATURU

Image
Na Mathias Canal, Ikungi-Singida Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Mhe. Miraji Mtaturu amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan inaendelea kuboresha Miundombinu mbalimbali kwenye shule ya Msingi Ikungi Mchanganyiko ili kurahisisha ujifunzaji na ufundishaji kwa watoto wenye mahitaji maalum ili kuweza kuongeza kiwango cha Elimu. Mbunge Mtaturu amesema hayo April 16, 2023 wakati akizungumza na watoto wenye mahitaji Maalumu baada ya kukagua miradi ya ujenzi wa Bwalo la chakula, Mabweni Mawili ya Wasichana na Wavulana ambapo serikali ya Rais Dkt. Samia imepeleka fedha Shilingi Milioni 300 kwa ajili ya ujenzi wa miradi hiyo. Mtaturu aliihakikishia kamati ya shule pamoja na walimu wa shule hiyo kuwa kupitia ofisi yake ataendelea kutatua changamoto mbalimbali kwa makundi yenye uhitaji ili kuboresha upatikanaji wa elimu kwa watoto hao. “ Nimshukuru Rais Samia ametuletea Milioni 300 kwaajili ya miradi ya ujenzi wa bw

TABASAMU LAONGEZEKA KWA WAKULIMA WILAYANI IKUNGI - SINGIDA

Image
Na Mwandishi wetu - Ikungi: Afisa Kilimo Ndugu Lucas Mkuki kutoka Sekretarieti ya Mkoa kwa niamba ya Katibu Tawala Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Singida awasisitiza wakulima kutumia mbinu za kisasa na kufuta kanuni bora za kilimo ili kufikia tija inayotakiwa katika kila mazao... Akizungumza katika Shehere ya Siku ya Mkulima Shambani iliyofanyika jana tarehe 06 April,2023 katika kijiji cha Matongo Meneja wa shirika hilo lisilo la kiserikali alisema wataendelea kufikia vijiji vingine na kutoa elimu hii lengo Ikiwa ni kukuza kilimo katika Wilaya ya Ikungi na Mkoa wa singida kwa ujumla... Naye Afisa kilimo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ndg Gurisha Msemo aliahidi kuendelea kufanya usimamizi wa hayo ili wakulima kuendelea kupata faida kubwa katika mradi huu wa Kilimo biashara "nitasimamia vikundi 40 ndani ya Wilaya yetu waliolima kwa tija ya kupata gunia 25 hadi 40 katika ekari 1" badala ya wakukima kulima kilimo cha mazoea.alisema Afisa Ki

TABASAMU LAONGEZEKA KWA WAKULIMA WILAYANI IKUNGI - SINGIDA

Image
Na Mwandishi wetu - Ikungi: Afisa Kilimo Ndugu Lucas Mkuki kutoka Sekretarieti ya Mkoa kwa niamba ya Katibu Tawala Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Singida awasisitiza wakulima kutumia mbinu za kisasa na kufuta kanuni bora za kilimo ili kufikia tija inayotakiwa katika kila mazao... Akizungumza katika Shehere ya Siku ya Mkulima Shambani iliyofanyika jana tarehe 06 April,2023 katika kijiji cha Matongo Meneja wa shirika hilo lisilo la kiserikali alisema wataendelea kufikia vijiji vingine na kutoa elimu hii lengo Ikiwa ni kukuza kilimo katika Wilaya ya Ikungi na Mkoa wa singida kwa ujumla... Naye Afisa kilimo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ndg Gurisha Msemo aliahidi kuendelea kufanya usimamizi wa hayo ili wakulima kuendelea kupata faida kubwa katika mradi huu wa Kilimo biashara "nitasimamia vikundi 40 ndani ya Wilaya yetu waliolima kwa tija ya kupata gunia 25 hadi 40 katika ekari 1" badala ya wakukima kulima kilimo cha mazoea.alisema Afisa Ki

ZIARA YA DC APSON, IKUNGI YAZIDI KUTATUA KERO, KUZINDUA NA KUTEMBELEA MIRADI

Image
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe. Thomas Apson amewataka wakandarasi kuzingatia ubora katika ujenzi wa miundombinu ya Serikali ili kuendana na wakati... Akizungumza mara baada ya kutembela Miradi mbalimbali leo tarehe 05 April 2023 ikiwemo shule ya Sekondari Mwau katika ujenzi wa maabara mbili za Kemia na biolojia zitakazogharimu Milioni 118.1,shule ya msingi Mwau katika ujenzi wa vyoo unalio fadhiliwa na Shanta Gold mine matundu 17 yaliyogharimu milion 46 pamoja na Zahanati ya Mang'onyi iliyogharimu Shilingi milioni 144.8 Mkuu wa Wilaya amewapongeza kwa hatua nzuri waliyoifikia na kushauri majengo yazingatie maagizo yanayotolewa na serikali... " Majengo lazima yawe yakisasa ili mtoto aweze kusoma katika mazingira yanayomvutia kuanzia sakafu,madirisha,rangi hata mabati yawe yakisasa ."alisema Mkuu huyo wa Wilaya ilaya... Kwa upande mwingine aliwapongeza Mgodi wa Shanta kwa kufadhili mradi wa vyoo pamoja na Zahanati ya Mang'onyi kwa kukamilika katika ubora na kuwaomba k

HALMASHAURI YA WILAYA YA IKUNGI YATOA MIKOPO YA 10% SHILINGI MILIONI 141 KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE MAHITAJI MAALUM

Image
Na Bazil Mjungu Singida: Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida imetoa mikopo ya asilimia kumi (10%) kutoka kwenye mapato yake ya ndani ya Shilingi milioni miamoja arobaini na Moja (141) na Verehani tatu katika Vikundi kumi na mbili vya Wanawake, Vijana na watu wenye mahitaji Maalum. Vikundi vilivyo nufaika ni Pamoja  na vya Wanawake ambavyo ni kikundi Cha Ushirika Cha Siuyu, Kikundi cha Jonelaa cha Siuyu, Kikundi cha Heshima Wanawake cha Ikungi, Tumaini Stara Cha Iyumbu, Kikundi cha Mshikamano cha Iyumbu, Kikundi cha Faraja cha Mgungira, Kikundi cha Igembensabo cha Ng'ongosoro, Kikundi cha Ipililo cha Ng'ongosoro sambamba na Vikundi vya Vijana ambavyo ni Kikundi cha Kidundu cha Kipunda, Kikundi cha Roho safi cha Iyumbu, Kikundi cha Be the Light cha Kipumbuiko, Kikundi cha Vijana Chapakazi cha Ikungi na Kikundi Cha Walemavu cha Kwajaa cha Matongo, Aidha, Mikopo hii imetolewa Leo February 7 kutoka kwenye nusu ya kwanza ya Bajeti ya Mwaka 2022/2023 Kama mchango wa asili

MASHINDANO YA MPIRA WA WAVU YA MAVUNDE CUP YAZINDULIWA RASMI LEO JIJINI DODOMA

Image
Na Mwandishi wetu Dodoma: Mashindano ya mpira wa wavu maarufu kama * MAVUNDE CUP * yamezinduliwa rasmi leo katika shule ya Msingi Mlezi Jijini Dodoma huku yakijumuisha Timu 18 za wanaume na wanawake kutoka mkoani Dodoma na nje ya Dodoma. Mashindano hayo yamezinduliwa leo na Diwani wa Kata ya Hazina * Mh. Samwel Mziba * akiongozana na Diwani wa Viti Maalum * Mh. Flora Lyacho * huku wote wakitoa rai kwa Vijana wa Dodoma kuchukua fursa ya haya mashindano kama sehemu ya kuendeleza na kukuza vipaji vyao. Aidha zoezi hili la uzinduzi wa mashindano limekwenda sambamba na ugawaji wa vifaa vya michezo kwa Timu zote zinazoshiriki katika mashindano hayo pamoja na ukarabati wa kiwanja cha kuchezea. Mashindano hayo yatafikia tamati tarehe * 01.01.2023 * siku ya Jumapili, ambapo Mgeni Rasmi wa mashindano hayo anatarajiwa kuwa * Mh. Anthony Mavunde * Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini na Mfadhili wa mashindano hayo. #bazotvnews.