Posts

Showing posts from December, 2019

MVUA YASABABISHA UHARIBIFU WA MASHAMBA YA KAYA 93 RORYA MARA

Image
Na_Bazil Mjungu. ROYRA MARA : Mvua iliyoambatana na upepo mkali iliyo nyeesha Desemba 12/2019 katika Kitongoji cha Sang'ombe Kijiji cha Tatwe Kata ya Goribe Wilayani Rorya Mkoani Mara imesababisha maporomoko makubwa ya mawe na mmomonyoko mkubwa wa ardhi hali iliyopelekea kuharibika kwa mashamba ya Kaya zaidi ya 93. Mbunge wa Jimbo la Rorya Mhe. Lameck Airo (CCM) alitembelea eneo hilo akiambatana na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Rorya, Charles Ochele na viongozi wengine wa Serikali za Vijiji na Kata kufika katika eneo la tukio na ujionea uharibifu mkubwa Mashamba kusombwa na Maji yenye Mawe Makubwa yaliyosababisha kutokea kwa mto na bonde kubwa huku za zaidi ekari 20 za mazao ya wananchi kusombwa na maji na kuharibiwa na mamia ya mawe yaliyoporomoka kutoka zaidi ya km 2 kutoka eneo la Mashamba n Mlima uliko. Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Tatwe Mhe. Lameck Airo ametoa pole kwa wananchi na kuonyesha kusikitishwa na tukio hilo ambalo limeacha maswali mengi na kuwashitua wananchi

ONA MADHARA YA KUMUAMSHA MDADA WA KAZI SAA 11 ALFAJIRI NA KUWAACHA BINTI ZAKO WAKILALA.

Image
Na Uhuru Kenyatta: Kumuamsha mdada wa kazi saa 11 alfajiri na kuwaacha binti zako wamelala Ni kumuandaa binti wa kazi kuwa mke Bora kuliko wanao.   Eti kumtumikisha dada wa kazi apige deki, apike, afue nguo, aoshe vyombo wakati wanao wanaangalia TV. Ni kumuandaa mdada wa kazi  kuwa mwanamke anayewajibika kuliko wanao. Kumuacha binti wa kazi aandae watoto kwenda shule, awaandalie uji mapema, awalishe, awasafishe wakati wanao wanacheza gemu kwenye simu au computer Ni kumuandaa binti wa kazi kuwa mama na mlezi bora kwa watoto kuliko wanao. Na kwakuwa yote hayo unayafanya kwa masimango na manyanyaso unamfanya mdada wa kazi kuwa jasiri mwenye kuzikabili changamoto za ndoa yake kuliko wanao. Ukimaliza kwa kusema mwanao akiwa hajui hayo yote, ndoa ikiharibika mnazunguka kutafuta maombi kwa wachungaji kumbe ninyi mmeharibu ndoa za watoto wenu. Msiwasumbue wachungaji. Rais Uhuru Kenyata. 🙏🙏🙏.

SIASA ZA IKUNGI NA HATIMA YA MAISHA YA WANAIKUNGI

Image
MAKALA YANGU: Ramadhani Ndoghwe: Jimbo la Singida Mashariki ni takribani miaka 9 limekuwa katika SIASA za UPOFU zisizokuwa na dhamira ya dhati kuwainua watu Kiuchumi na kijamii huduma za Afya na Maji zilikosekana kwa %70, Barabara hazikupitika, Vijana walikaririshwa kuwa maendeleo ni Kuku kuota Makucha  eti hayo ndio maendeleo wakasahau kuwa MTU NI AFYA, wakasahaulishwa Ukombozi FIKIRA CHANYA  na kushiriki kikamilifu katika kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais John Pombe Magufuli za Tanzania ya Viwanda na Uchumi wa kati. Mnamo September 2019 alipatikana Mbunge mwenyewe dahana halisi ya kuwasemea wananchi na kuleta chachu ya maendeleo katika Jimbo la Singida Mashariki na Vitu kama Miundombinu za Barbara, Maji na Afya zimeanza kutatulia na kuonyesha njia sahihi ya maana ya uongozi niseme Sasa tumetoka kule tulipokuwa na sasa tunaenda kutekeleza dhana hizo kikubwa ni kuamini kuwa TANZANIA ya Viwanda inawezekana Kwa sasa Jimbo la Singida Mashariki, Tumepata Mhe. Miraji Mtaturu kiongozi mwenye