Posts

Showing posts from September, 2021

BARABARA YA MUNGAA - NTUNTU MATENGENEZO YAANZA MILIONI 152 KUTUMIKA

Image
Katika Jimbo la Singida Mashariki, Hatimaye Serikali yaanza Matengenezo ya Barabara ya Mungaa - Ntuntu Shilingi Millioni 152 Kutumika.

FUNGUO SABA ZA KUKUZA KIWANGO CHAKO NA MUNGU ( SEVEN KEY TO RAISE YOUR PERSONAL LEVEL WITH GOD.)

Image
Na Mwinjilisti: Musa Njagamba Kitabu cha Yoshua 1:8 8 Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana. Tunachokiona hapa ni msisitizo wa Mungu kumsisitiza Nabii Joshua juu ya kulitafakari NENO la Mungu, Usiku Na Mchana. Kusudi la Waraka huu Au Ujumbe huu ni kutusaidia sisi wasomaji kujua nini ni lazima katika Maisha yetu Na wala sio ombi kwamba Tusome Na kulitafakari Neno la Mungu Usiku Na mchana. Tafsiri yake hapa juu ya NENO la MUNGU kwa ufupi ni kwamba ni Jumla ya Mawazo ya Mungu juu ya Mwanadamu. ➡️Ndani ya NENO la Mungu kuna Maamuzi ,( Hukumu) sheria. Maaagizo Na Njia za Mungu za kumtoa mwanadamu katika Shida aliyonayo Na kila Aina ya changamoto anayopitia Ili kumfanikisha katika mambo yote Na kukusaidia katika mambo yote ili kuishi la kulishika shauri lake ( kusudi la Bwana.)

SHIRIKA LA RESTLESS DEVELOPMENT TANZANIA LAWAFUNGULIA NJIA VIJANA WAJASIRIAMALI MKOANI SINGIDA.

Image
Na Bazil Mjungu Singida. Shirika la Restless Development Tanzania likiongozwa na Mkurugenzi Mkuu Bi. Haika, Meneja wa Miradi Bw. Ridhione Juma na Afisa mawasiliano wa shirika hilo wakiambatana na Saimon Sirilo Mratibu wa Vikundi vya Ujasiriamali kwa vijana Mkoa wa Singida. Wamewatembelea Vijana walionufaika na mafunzo ya Ujasiriamali yaliyotolewa na Shirika Hilo. Wilaya ya Ikungi na Itigi Mkoani humo Vijana wa Vikundi vya Ufugaji Nguruwe wa kisasa kutoka Mwisi, Kikundi cha Chaki kilichopo Mwisi, Kikundi cha Tofali Cha Puma na kikundi cha Tofali Ikungi. Vijana hao wamekiri kunufaika na mafunzo hayo na kusema mafunzo hayo yamewasaidia kufika mahali kwa kuanzisha Vikundi, kusajili na kupata Mikopo kutoka Halmashauri wanazo ishi. Aidha, Shirika limewasaidia Fedhaza chakula na usafiri uliowawezesha kushiriki kikamilifu mafunzo hayo. Uongozi wa shirika umewapongeza Viongozi wa Serikali kuanzia ngazi ya Vijiji, Kata na Halmashauri kwa kushikamana na shirika hilo toka mwanzo hadi mwisho wa maf

RAIS SAMIA ADHAMIRIA KUENDELEZA KILIMO NCHINI - MAJALIWA

Image
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuendeleza kilimo cha mazao ya chakula na biashara ili kuhakikisha nchi inakuwa na uhakika wa usalama wa chakula na ziada kuuza nje. Ameyasema hayo leo (Alhamisi, Septemba 16, 2021) baada ya kukagua shamba la michikichi la kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) 821 KJ Bulombora akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo mkoani Kigoma.   Amesema Serikali inatekeleza dhamira hiyo kwa kufuatilia kwa ukaribu kilimo cha mazao hayo likiwemo na la michikichi kuanzia hatua za awali za utayarishaji wa shamba hadi upatikanaji wa pembejeo. “Wazazi waanzishieni watoto wenu mashamba ya michikichi kwa ajili ya kuwakwamua kiuchumi ili wasiwe tegemezi.”   Mheshimiwa Majaliwa ametumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi hususani waliopo kwenye mikoa inayolima michikichi washiriki katika kilimo cha zao hilo kwa ajili ya kuku