Posts

Showing posts from December, 2021

TANZANIA IKO MIKONONI MWA MUNGU: WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA

Image
Na: Bazil Mjungu - Lindi. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amesema Tanzania iko mikononi mwa Mungu na ndiyo maana imeendelea kuwa nchi yenye amani na utulivu na kimbilio la mataifa yaliyopoteza tumaini. “Nchi hii imeshikwa na Mwenyezi Mungu na ni kwa sababu viongozi wa dini wanaendelea kuliombea Taifa hili, kwa hiyo na sisi tunalo jukumu la kuhakikisha kwamba nchi hii inabaki kwa salama,” Waziri Mkuu. Mhe. Majaliwa Ametoa kauli hiyo leo mchana (Ijumaa, Desemba 31, 2021) wakati akizungumza na waumini baada ya kushiriki ibada ya Ijumaa na kuzindua msikiti wa Nkowe, ulioko kata ya Nkowe, wilayani Ruangwa, mkoani Lindi. Amesema Serikali zote tangu awamu ya kwanza hadi ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, zimeendeela kuheshimu uwepo wa dini nchini kwani miongozo na mafundisho yanayotolewa na viongozi wa dini mbalimbali yanawafanya waumini wao kuwa raia wema. “ Mheshimiwa Rais alipoingia madarakani alikutana na Mababa Askofu wote

MTATURU JIMBO CUP YAHITIMISHWA RASMI NA WAZIRI WA SANAA, UTAMADUNI NA MICHEZO MHE. INNOCENT BASHUNGWA

Image
Na Bazil Mjungu Singida: Waziri wa Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe Innocent Bashungwa leo Tarehe 26/12/2021 Amehitimisha Rasmi Mashindano ya Mpira wa Miguu yaliyojulikana Kama Mtaturu Jimbo Cup Katika Uwanja wa Sekondari Ikungi, Katika Jimbo la Singida Mashariki Wilayani Ikungi, Ambapo Katika Kuhitkmisha ligi hiyo kulikua na Mechi ya Fainali iliyohusisha timu ya Mampando Fc na Matongo Fc ambambo mechi iliisha kwa Dakika 90 kwa Timu ya Matongo Fc kuibuka dhidi ya Mampando Fc. Waziri Bashungwa ameonyesha kufurahishwa na Taarifa ya Mashindano hayo na kumpongeza mdhamini wa ligi hiyo Mhe. Miraji Mtaturu kwa jitihada zake za kuwaletea wananchi maendeleo Jimboni humo. " Kipekee niseme tu niwe mshuhuda hata Bungeni Mhe. Mtaturu amekua akijenga hoja zenye masilahi kwa wananchi wake na hata akiomba Mradi unaohusu Jimbo Basi ukiwa Waziri wa Wizara aliyoomba Jambo utamuona akifuatilia Hatua zote ili Kuhakikisha alichokiomba kinawafikia Wananchi wake" Alisema Mhe. Bashungwa Aidha, Mhe. B

MTATURU ACHANGIA VYEREHEANI 10 CHUO CHA KIISLAM - JIMBONI

Image
Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Mhe. Miraji Mtaturu ameshiriki Sherehe za Maadhimisho ya kutimiza Mwaka Mmoja tangu kuanzishwa kwa Chuo cha Kiislamu Cha (Almadrasatul Tah Dhiibul Islaamiyaa) kilichopo Kata ya Dung'unyi Wilayani Ikungi Singida Ambapo amewaomba Viongozi wa Dini kuhubiri Umoja na mshikamano. Mbungehuyo baada ya kuwasili na kujionea Mazingira ya Wanafunzi wanayojifunzia alionyesha kufurahishwa na usimamizi wa Chuo hicho ambapo bila kumumunya maneno aliamua kutamka kuchangia Vyerehani 10 na Seti moja ya Ufundi Seremala ili kuwafanya Wanafunzi kusoma kwa vitendo na wakimaliza masomo yao wakawe mfano Bora kwa familia zao. Akizungumza Katika Hafla hiyo ya Maadhisho Mhe. Mtaturu akasema Nimefurahishwasana na mafunzo haya mnayofundishwa hapa Vijana,  na Ninataka niwaambieni kila mtu anapaswa kujua wakati upi wa kujiandaa kimasomo na wakati upi wa kupoteza, na Ninataka niwahimize wazazi na walezi wa hawa Wanafunzi hakuna kitu kizuri Kama kumuunga mkono mtoto ukigundua an